Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Bashiru: Kweli vyuma vimekaza
Habari za Siasa

Dk. Bashiru: Kweli vyuma vimekaza

Spread the love

DAKTARI Bashiru Ally, Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), amesema “ni kweli vyuma vimekazi” akaongeza “kwa wale wapiga dili.” Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kiongozi huyo wa chama tawala, yumo jijini Dar es Salaama akiendelea na ziara yake ya kichama katika Jimbo la Ubunge linaloongozwa na Saed Kubenea (Chadema) ikiwa ni siku yake ya pili.

Akizungumza leo tarehe 28 Agosti 2019 katika Shule ya Msingi Ubungo Kisiwani Dk. Bashiru amesema, ni wakati wa kufanya kazi na sio kukaa ‘vijiweni’ kwamba wale wasiokuwa na kazi maalumu wataendelea kulalamika.

“Vijana waachane na tabia ya uvivu kwani uvivu ni adui wa maendeleo… muda wa kupata dezo umepita,” amesema Dk. Bashiru na kuongeza; “vijana muache kukatishana tamaa.”

Amesema, ikiwa vyuma vimekazwa kwa sababu ya kujenga shule, kuokoa vifo vya kina mama, kulina uhuru na amani bado vyuma hivyo viendelee kukaza mpaka Watanzania tushike adabu.

Dk. Bashiru anaendelea na ziara yake kwenye jimbo hilo, ambapo baadaye ataanza ziara katika jimbo la Kibamba linaloongozwa na John Mnyika (Chadema).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!