MUSTAFA Muro, aliyekuwa Diwani wa Kinondoni, jijini Dar es Salaam kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ameomba ridhaa ya kugombea ubunge katika Jimbo la Kinondoni kupitia Chama cha NCCR-Mageuzi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).
Muro ambaye anamaliza muda wake wa udiwani, ametangaza nia hiyo leo Jumatano tarehe 24 Juni 2020, wakati akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam.
Pia amesema, Martha Chilomba, aliyekuwa mwanachama wa Chadema, ametia nia ya kugombea Jimbo la Kawe, jimbo hilo limeongozwa na Halima Mdee (Chadema) kwa miaka 10 (2010-2020).
“Mimi Mustapha Muro, nimetia nia kugombea Kinondoni, bahati mbaya mwenzangu wa Kawe, Martha Chilomba, amepata msiba na ameenda Tabora, pamoja na sisi hapa tunao watia nia wa udiwani,” amesema Murro.
Leave a comment