Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko DIT inavyojipanga kukabili soko la ajira
Habari Mchanganyiko

DIT inavyojipanga kukabili soko la ajira

Spread the love

TAASISI ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) inakusudia kuboresha mitaala ya shahada mbili za umahiri (masters) ili kuendana na ushindani wa soko la ajira ndani na nje. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Pia, lengo la maboresho hayo ni kuwawezesha wahitimu kuwa na uwezo mkubwa ikiwemo kujiajiri.

Jana Jumanne tarehe 11 Agosti 2020, DIT ilikutana na wadau mbalimbali ili kujadiliana jinsi ya kuboresha mitaala hiyo.

Shahada zinazoboreshwa ni Master of Computational Science and Engineering-MCSE na Master of Maintenance in Engineering and Management-MENG).

Mkuu wa Idara ya Masomo ya Umahiri, Utafiti na Machapisho wa DIT, Profesa Leonia Henry, anasema kuwa wataangalia eneo la ufundishaji, vifaa vinavyotumika kufundishia na maendeleo ya kidijitali.

“Mchakato huu ukikamilika, mitaala iliyoboreshwa itaanza kutumika katika mwaka mpya wa masomo unaonza Novemba 2020,” alisema Profesa Leonia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!