Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Dereva wa mbunge auwawa na polisi
KimataifaTangulizi

Dereva wa mbunge auwawa na polisi

Spread the love

DEREVA wa Mbunge wa Jimbo la Kyaddondo Mashariki  nchini Uganda,  Robert Kyagulanyi  Bobi Wine, Yasin Kawuma amefariki baada ya kupigwa risasi na watu wanaodaiwa kuwa na polisi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Bobi Wine amedai kuwa dereva wake ameuawa kwa kupigwa risasi na polisi akiwa ndani ya gari la mbunge huyo, wakidhani kuwa aliyekuwa kwenye gari ni yeye.

Mbunge huyo ambaye pia ni msanii wa muziki nchini humo, ameandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter kuwa walikuwa eneo linalojulikana kama Arua kwenye kampeni wakati mauaji hayo yalitokea.

Bobi Wine na viongozi kadhaa wa upinzani walikuwa eneo hilo kumuunga mkono mgombea huru Kassiano Wadri anayeshiriki katika uchaguzi mdogo wa kuziba nafasi ya Mbunge wa jimbo hilo, Ibrahim Abiriga aliyeuawa.

Wakati wa kampeni hizo zikiendelea kulizuka vurugu kati ya wafuasi wa Wadri na wale wa mpinzani wake katika uchaguzi huo wa chama cha NRM, Tiperu Nusura.

Msemaji wa polisi Emilian Kayima, anasema watu waliokuwa wamevaa shati za kampeni za mgombea Wadri, walianza kuurushia mawe msafara wa rais hali ambayo ilisababisha polisi kufyatua risasi.

“Mwendo wa saa kumi na mbili jioni msafara wa rais ulishambuliwa na wahuni katika manispaa ya Arua wakati rais alikuwa anaondoka uwanja wa Boma ambapo alikuwa amefanya mkutano wa mwisho,” amesema Kayima.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Deni la Serikali laongezeka kwa trilioni 11

Spread the loveDENI la Serikali imeongezeka kwa takribani Sh. 11 trilioni sawa...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari MchanganyikoTangulizi

Baba aomba msaada kuzika miili ya familia yake iliyofunga bila kula kuonana na Mungu

Spread the loveWAKATI Mamlaka nchini Kenya, ikiendelea kukabidhi miili ya watu waliofariki...

error: Content is protected !!