Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa DC mwingine afariki dunia Tanzania
Habari za Siasa

DC mwingine afariki dunia Tanzania

Seleman Jafo
Spread the love

HAMIM Gwiyama, Mkuu wa Wilaya (DC) wa Nyang’hwale mkoani Geita amefariki dunia. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa iliyotolewa na Rebecca Kwandu, Mkuu wa KItengo cha Mawasiliano wa Ofisi ya Rais- Tamisemi imemnukuu Waziri wa Tamisemio, Seleman Jafo akitangaza kifo cha Gwiyama kilichotokea leo Alhamisi tarehe 7 Mei 2020 saa 5 asubuhi katika Hospitali ya Rufaa Bugando baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Waziri Jafi amesema DC huyo aliongoza wizara hiyo tangu tarehe 26 Juni 2016 alipoteuliwa na Rais John Pombe Magufuli.

Katika taarifa hiyo, Waziri Jafo amemtumia salamamu za rambirambi mkuu wa mkoa wa Geita, Robert Gabriel, wananchi wa wilaya hiyo, ndugu, jamaa na wote walioguswa na msiba huo.

Kifo cha Gwiyama kimetokea ikiwa ni takribani siku kumi tangu Evod Mmanda, aliyekuwa

Mkuu wa Wilaya ya Mtwara  kufariki dunia, tarehe 27 Aprili 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!