Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Dawasa yatangaza upungufu wa maji saa 24 Dar
Habari Mchanganyiko

Dawasa yatangaza upungufu wa maji saa 24 Dar

Bomba la maji safi
Spread the love

MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (Dawasa), imetangaza upungufu wa huduma ya maji kwa baadhi ya wananchi wa Jiji la Dar es Salaam kuanzia leo Jumanne hadi kesho Jumatano tarehe 6 Januari 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Taarifa iliyotolewa leo Jumanne na Kitengo cha Mawasiliano na Jamii-Dawasa imesema, sababu inatokana na usafishaji wa machujio ya maji  hali itakayosababisha upungufu wa uzalishaji maji kwa asilimia 25 na kuathiri huduma ya maji kwa saa 24.

Dawasa imeyataja maeneo yatakayoathirika ni: Mji wa Bagamoyo, Vijiji vya Zinga, Kerege, Mapinga, Bunju, Boko, Kawe, Kinondoni, Ilala, Temeke, Uwanja wa Ndege na Tegeta, Kunduchi na Salasala.

Maeneo mengine ni, Jangwani, Mbezi Beach, Mlalakuwa, Mwenge, Mikocheni, Msasani, Sinza, Kijitonyama, Oysterbay, Magomeni, Upanga, Kariakoo, City Centre, Ilala, Ubungo Maziwa, Kigogo, Mburahati, Hospitali ya Rufaa Muhimbili na Kigamboni Navy na Ferry.

“Dawasa inaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza,” inaeleza taarifa hiyo

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!