Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Dawa za nguvu za kiume zateka Bunge
Habari Mchanganyiko

Dawa za nguvu za kiume zateka Bunge

Jengo la Bunge la Tanzania mjini Dodoma
Spread the love

MBUNGE wa Konde,Khatibu Haji (CUF) amedai kuwa tatizo la upungufu wa nguvu za kiume limekuwa likiwasumbua Watanzania wengi na kuihoji serikali kama kuna hatua inachukua ili kukabiliana na tatizo hilo, anaandika Dany Tibason.

Akiuliza swali la nyongeza leo bungeni,Haji alidai kuwa tatizo hilo pia limekuwa likiwasumbua baadhi ya Wabunge kwani wamempelekea waraka (memo) wakieleza shida zao juu ya tatizo hilo.

“Mheshimiwa Spika hapa katika meza yangu nina ‘memo’ chungu nzima kutoka kwa waheshimiwa wabunge akiwemo Rashid Shangazi, Joseph Selasini, wote wakielezea shida ya jambo hili,” amesema

“Mheshimiwa Spika hivi sasa kuna utitiri wa matangazo ya biashara ya dawa za kuongeza nguvu za kiume kuna matangazo mengi yanatolewa na kusambaa nchini, jambo ambalo linaashiria ukubwa wa jambo hilo.

“Je Wizara inachukua hatua gani zinazochukuliwa kuhusu utumiaji wa dawa kiholela.

“Mheshimiwa Naibu Spika tendo la raha linahitaji furaha kuna taasisi imeeleza kuwa Tanzania ni mojawapo ya nchi 10 duniani ambayo wananchi wake wamepoteza furaha.

“Sasa ni miaka 50 ya uhuru, je Serikali kwanini nchi yetu iko katika nafasi ya 10 mwisho duniani kwa kupoteza furaha mmekosea wapi,? alihoji Mbunge huyo.

Akijibu swali hilo,Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto,Dk.Hamisi Kigwangala alikiri Watanzania wengi kusumbuliwa na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari Mchanganyiko

GGML yasisitiza kuendelea kuimarisha afya za wafanyakazi

Spread the loveKAMPUNI ya Geita Gold Mining Limited kwa kushirikiana na kampuni...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

error: Content is protected !!