Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Dawa za kulevya, utakatishaji fedha zamkaba koo kortini
Habari Mchanganyiko

Dawa za kulevya, utakatishaji fedha zamkaba koo kortini

Spread the love

ABUU Kimboko, Mkazi wa Mbagala Rangitatu, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam kwa mashtaka mawili, likiwemo la kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya aina ya Heroin. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam…(endelea).

Akisomewa mashtaka hayo na wakili wa serikali Elia Atanus, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Salum Ally leo tarehe 14 Januari 202, Kimboko anadaiwa tarehe 29 Desemba 2019, katika maeneo ya Mbagala Zakhiem, alijihusisha na biashara ya dawa za kulevya aina ya Heroin yenye uzito wa gram 273.45.

Pili; anakabiliwa na shitaka la utakatishaji fedha, ambapo inadaiwa kati ya tarehe 1 – 29 Desemba 2019 alijipatia kiasi cha Sh. 990,000 huku akifahamu fedha hizo ni zao la biashara haramu ya dawa za kulevya.

Wakili Atanus amedai, upelelezi wa shauri hilo upo mbioni kukamilika. Mtuhumiwa hakutakiwa kujibu chochote kwasababu, mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza kesi ya uhujumu uchumi. Kesi imeahirishwa hadi tarehe 28  Desemba 2020 ambapo itakuja kutajwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Puma Energy Tz: Watanzania tudumishe amani kuvutia uwekezaji

Spread the loveKAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika...

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!