Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo David Kameta asaini Simba
Michezo

David Kameta asaini Simba

Spread the love

KLABU ya Simba imemsajiri aliyekuwa beki wa Lipuli FC, David Kameta, kwa mkataba wa miaka miwili kwa ajili ya kuimalisha kikosi chao kuelekea msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara unaotarajia kuanza 6, Septemba, 2020. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Kameta amejiunga na Simba baada ya kuonesha kiwango bora kwenye michezo ya ligi kuu akiwa na kikosi cha Lipul kutoka mkoani Iringa ambayo kwa sasa imeshuka daraja.

Usajili wa mchezaji huyo umetangazwa leo kupitia mitandao yao ya kijamii ambayo toka jana imeanza kutambulisha wachezaji wapya watakaotumikia timu hiyo kwa msimu ujao.

Kusajiliwa kwa Kameta kutaenda kutia chachu kwenye eneo la ulinzi wa upande wa kulia ambao kwa sasa lipo chini ya Shomari Kapombe ambaye amekuwa kwenye kiwango bora toka aliporudi kwenye timu hiyo akitokea Azam FC.

Mpaka sasa klabu ya hiyo imeshasajili wachezaji wanne toka kufunguliwa na dirisha kubwa la usajili 1 Agosti, 2020 ambalo litadumu kwa kipindi cha mwezi mmoja tu.

Wachezaji wengine waliosajiliwa na klabu hiyo mpaka sasa ni Bernad Morrison kutoka Yanga, Joash Onyango kutoka Gor mahia,Charles Ilamfia aliyekuwa kmc na beki aliyekuwa anacheza Costal Union Ibrahim Ame.   

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!