BARAZA kuu la uongozi la Chama cha Wananchi (CUF), linakutana mchana huu mjini Zanzibar kwa lengo la kujadili mgogoro unaondelea ndani ya Chama hicho, anaandika Hamisi Mguta.
Baraza hilo ambalo ndilo chombo kikuu cha kutoa maamuzi kinatarajia kujadili masuala mbalimbali hususani yanayohusu kuvuliwa uanachama wanane kulikofanywa na mwenyekiti Prof. Ibrahim Lipumba anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi.
Wabunge waliotenguliwa nafasi zao ni Severina Mwijage, Saumu Sakala, Salma Mwassa, Riziki Ngwali, Raisa Mussa, Miza Haji, Hadija Al-Qassmy na Halima Mohamed. Wakati huo kesi mbalimbali zilizotokana na Mgogoro baina ya pande hizo mbili zikiwa zinaendelea Mahakamani.
MwanaHALISI Online itakujulisha zaidi kutoka katika mkutano huo baadaye…..
Leave a comment