Thursday , 18 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CUF watoa msimamo madiwani wake kuhama
Habari za Siasa

CUF watoa msimamo madiwani wake kuhama

Maalim Seif Sharif Hamad, Katibu Mkuu wa CUF. Picha ndogo Prof. Ibrahim Lipumba
Spread the love

CHAMA cha Wananchi (CUF) kimetoa msimamo wake kuhusu kuhama kwa waliokuwa viongozi, wabunge na madiwani wa chama hicho, kikisema kuwa kitafanya vikao vyake vya kitaifa hivi karibuni ili kujaza nafasi wazi za uongozi zilizokuwepo. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea). 

Msimamo huo wa CUF umetolewa leo tarehe 19 Agosti, 2018 na Naibu Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano, Mbarala Maharagande, akisema kwamba chama hicho kitaitisha vikao vya Kamati ya Utendaji ya Taifa na Baraza Kuu la Uongozi la Taifa ili kufanya tathmini ya pamoja na kuweka mikakati thabiti ya kuendeleza mapambano ya kisiasa, kukilinda Chama na kujaza nafasi wazi za Uongozi zilizokuwepo.

Julius Mtatiro aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya CUF Taifa ni miongoni mwa watu waliohama chama na kujiuzulu vyeo vyao, wengine ni Maulid Mtulia aliyekuwa Mbunge wa Kinondoni, na Mussa Kafana aliyekuwa Naibu Meya wa Jiji la Dar es Salaam.

Kuhusu kauli ya CUF juu ya wabunge, madiwani na viongozi wake waliohama, Maharagande amesaema chama hicho hakina pingamizi kwa kiongozi au mwanachama yeyote pale atakapoona ameshindwa kusimamia malengo na madhumuni ya chama hicho, kujiondoa ndani ya chama.

Hata hivyo, Maharagande amesema hoja zilizowapelekea kuhama hazina mashiko na kwamba wametanguliza masilahi yao binafsi. Na hivyo kitendo hicho kinawapa fursa nzuri ya kujipanga upya kwa kuwa na wapambanaji sahihi kwenye nafasi husika.

“Kumezuka taharuki kwa wanachama wetu na Watanzania wapenda Mabadiliko nchini kufuatia baadhi ya Viongozi wa Chama kwa nafasi za Kiserikali, madiwani na Wabunge kujiuzulu nafasi zao na kujiunga na CCM.

Hakuna sababu ya kutaharuki zaidi ni kuwaonea huruma kwa sababu wamekubali kujivunjia heshima zao mbele ya jamii iliyowaamini na kuwa watumwa wa kifikra,” amesema Maharagande.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

error: Content is protected !!