Tuesday , 23 April 2024
Kimataifa

Corona yatua Kenya

Mutahi Kagwe, Waziri wa Afya Kenya
Spread the love

KENYA inakuwa nchi ya kwanza katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kuripotiwa kugundulika kwa mtu mwenye virusi vya Corona (COVID-19, mamlaka ya nchi hiyo imethibitisha. Inaripoti mitandano ya kimataifa … (endelea).

Leo tarehe 14 Machi 2020, Mutahi Kagwe  ambaye ni Waziri wa Afya nchini humo, amewaeleza wananchi wa taifa hilo kwamba, mgonjwa wa kwanza tayari ameripotiwa.

Amesema, Mkenya mmoja aliyetoka nchini Marekani kupitia London, Uingereza na kwasili nchini humo tarehe 5 Machi 2020, amekutwa na virusi hivyo.

”Tarahe 5 mwezi Machi aligunduliwa kuwa na virusi hivyo katika maabara ya serikali, lakini sasa viwango vyake vya joto vimeshuka na kuwa vya kawaida.

“Anakula vizuri lakini hawezi kutolewa hadi virusi hivyo vitakapokwisha mwilini,” amesema.

Waziri huyo amesema, kwamba kisa hicho ni cha kwanza kuripotiwa nchini Kenya tangu kuzuka kwa mlipuko huo mjini Wuhan, China.

Kagwe  amesema, kwamba mgonjwa huyo ambaye ni mwanamke, yuko katika hali njema. Pia amewataka Wakenya kuwa watulivu na kutokuwa na wasiwasi.

Amesema kwamba serikali ya Kenya kupitia wizara ya afya itaendelea kuimarisha mikakati ili kuhakikisha kwamba hakuna usambazaji wa virusi hivyo zaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!