Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Corona: Waziri Mkuu wa Uingereza hoi, akimbizwa hospitali
Afya

Corona: Waziri Mkuu wa Uingereza hoi, akimbizwa hospitali

Boris Johnson, Waziri Mkuu wa Uingereza
Spread the love

BORIS Johnson, Waziri Mkuu wa Uingereza amekimbizwa hospitali kutokana na makali ya virusi vya corona (COVID-19). Linaripoti Shirika la Habari la BBC.

Boris alikimbizwa hospitali jana Jumapili usiku katika hospitali moja ya mjini London. Amepelekwa ikiwa ni siku 1 baada ya kubainika kuwa na maambukizi ya virusi hivyo alipokuwa ofisini kwake Downing Street.

Hatua hiyo imechukuliwa baada ya joto mwilini kupanda zaidi, meonekana. Kutokana na joto hilo, daktari wa Boris alishauri apelekwe hospitali.

Kutokana na hatua hiyo, waziri wa maswala ya kigeni nchini humo, Jeremy Hunt anatarajiwa kuongoza mkutano wa virusi vya corona leo.

Ijumaa wiki iliyopita Boris aliandika kwenye ukurasa wake wa twitter “Bado nina joto mwilini. Hivyo basi kulingana na ushauri wa serikali, ninafaa kuendelea na karantini hadi pale dalili hizo zitakapopotea,’ na kuongeza ”hata hivyo, tunafanya kazi muda wote ili kuvishinda virusi hivi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!