Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Corona sasa yamkumba mbunge wa Tanzania
Habari za SiasaTangulizi

Corona sasa yamkumba mbunge wa Tanzania

Spread the love

NAIBU Spika wa Bunge la Jamhuri, Dk. Tulia Akson, amelitangazia Bunge kuwa mmoja wa wabunge wa Bunge hilo, amepatwa na virusi vya Corona. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea). 

Akizungumza bungeni mchana huu, muda mfupi kabla ya kughairisha Bunge, Dk. Tulia alisema, mbunge huyo alithibitika kuwa na ugonjwa huo, mwishoni mwa wiki iliyopita.

Naibu Spika Tulia, hakutaja jina la mbunge ambaye amesema ameambukizwa virusi hivyo.

Hata hivyo, baadhi ya wabunge wamemwambia mwandishi wa habari hizi kuwa mbunge huyo anatokea moja ya majimbo ya mkoa wa Dar es Salaam.

Alisema, “tumepata taarifa kuwa mbunge mwenzetu alikuja Dodoma kutokea Dar es Salaam, Jumatano iliyopita. Akiwa hapa Dodoma akaanza kujisikia vibaya na hivyo akalazimika kurudi Dar es Salaam

“Alipofika Dar es Salaam akaenda hospitali ambako baada ya kufanyiwa uchunguzi na madaktari bingwa wanaojihusisha na ugonjwa huu, amethibitika kuwa na maambukizi.”

Dk. Tulia alitoa tangazo hilo, wakati akighairisha Bunge kupisha msiba wa mbunge wa Viti Maalum (CCM), Gerturde Pangalile Rwakatare.

Mbunge Rwakatare ambaye ni Askofu wa Kanisa la Assembliess of God – maarufu kama Mlima wa Moto – alikutwa na mauti asubuhi ya kuamkia leo Jumatatu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!