Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Corona janga la dharura – WHO
Kimataifa

Corona janga la dharura – WHO

Spread the love

TEDROS Adhanom, Kiongozi Mkuu wa Shirika la Afya duniani (WHO), ametangaza kwamba virusi vya Corona sasa ni janga la dharura duniani. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Adhanom amesema “watu takribani 213 wamefariki kutokana na virusi hivyo nchini China.”

Amesema, WHO limedhibitisha, kwamba kumekuwa na visa 98 katika mataifa mengine 18 ingawa hakuna vifo virivyoripotiwa. Visa vingi vya wagonjwa hao vilitokana na watu waliosafiri kutoka mji wa Wuhan, China eneo ambalo mlipuko wa ugonjwa huo ulipoanzia.

“Sababu kubwa ya tangazo hilo si kwa sababu ya kile ambacho kinatokea China kwa sasa, lakini kile ambacho kinatokea katika mataifa mengine,” amesema Adhanom.

Hata hivyo, Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya nchini Tanzania amesema, mtu yeyote atakayepata virusi vya Corona ndani ya Tanzania, atatibiwa katika maeneo yaliyotengwa yaliyopo mkoani Kilimanjaro, Dar es Salaam na Mwanza na kwamba, mpaka sasa hakuna mkasa wa virusi hivyo nchini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!