JUMLA ya wanachuo 3,421 wamehitimu masomo yao katika Chuo cha Diplomasia tangu kuanzishwa kwake mwaka 1978. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).
Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 23 Aprili 2019 na Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrka Mashariki, Damas Ndumbaro wakati akijibu swali la Mbunge wa Malindi, Ally Salehe Ally (CUF).
Katika swali lake Salehe alitaka kujua Chuo Cha Diplomasia kimetoa wahitimu wangapi tangu kuanzishwa kwake mwaka 1978?
Ndumbaro amesema, wahitimu wa ngazi ya Shahada ni 72, Stashahada ya Uzamili katika Menejimmenti ya Mahusiano ya kimataifa ni 503, Shahada uzamili katika Diplomasia ya Uchumi ni 341, Stashahada ya kawaida 2084, ngazi ya cheti ni 347 ni wa mafunzo maalum ya maafisa waandamizi wa Mambo ya Nje.
Amesema, katika idadi hiyo ya wahitimu katika Chuo cha Diplomasia wanawake 1,060 na wanaume 2,361.
Naibu huyo amesema, wanafunzi hao walitoka nchi mbalimbali ikiwemo Afrika Kusini, Algeria, Angola, Butswana, Burundi, Jamhuri ya Kongo, Guinea, Kenya. Comoro, Libya, Malawi na Msumbiji.
Nchi zingine ni pamoja na Namibia, Palestina, Rwanda, Sudan, Zambia, Zimbabwe pamoja na hapa nchini.
Amesema kuwa, tangu kuanzishwa kwa chuo hicho mpaka sasa, wanachuo 500 kutoka Tanzania wamehitimu na kufanya kazi katika maneo mbalimbali ndani na nje ya nchi.
Na kwamba, kutokana na umuhimu wa lugha za kufundishia, chuo kwa sasa inafundisha kwa kutumia ya lugha mbalimbali za kigeni katika kufundishia.
Ametaja lugha hizo kuwa ni pamoja na Kifaransa, Kihispania, Kingerreza, Kikorea na Kireno.
Leave a comment