MSHAMBULIAJI wa zamani wa Yanga, Obrey Chirwa amejiunga rasmi na klabu ya Azam FC kwa mkataba wa mwaka mmoja katika dirisha dogo la usajili akitokea Nagoom El Mostakbal FC ya Misri baada ya kuvunja mktaba wake. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea)
Chirwa ambaye hapo awali alitaka kurudi kwenye klabu yake ya Yanga ila kocha mkuu wa timu hiyo Mwinyi Zahera aligomea swala hilo kwa sababu ya kumuona mchezaji huyo yupo kimaslahi zaidi.
Mshambuliaji huyo ambaye alikuwa kinara wa ufungaji ndani ya kikosi cha Yanga katika msimu wa 2017/18 anakwenda kuongeza nguvu ndani ya kikosi cha Azam FC ambacho kinaongozwa na kocha Hans Van Pluijm.
Leave a comment