Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa China yashukiwa kupotea kwa Rais wa Interpol
KimataifaTangulizi

China yashukiwa kupotea kwa Rais wa Interpol

Rais wa Shirika la Polisi la Kimataifa (Interpol), Meng Hongwei
Spread the love

UTATA umeibuka kufuatia madai ya kupotea kwa Rais wa Shirika la Polisi la Kimataifa (Interpol), Meng Hongwei baada ya  Afisa Mkuu wa masuala ya sheria nchini Ufaransa kukana kwamba kiongozi huyo hakuwa nchini humo wakati alipopotea. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Wakati hayo yakijiri kwa mujibu wa gazeti la South China Morning Post  la Hong Kong, liliripoti kuwa Hongwei  yuko ndani ya uchunguzi nchini humo kwa sababu zisizojulikana, huku likiadai kwamba, Mkuu huyo wa Interpol ambaye aliwahi kuwa naibu waziri wa usalama wa umma China alichukuliwa na vyombo vya dola kwa ajili ya kuhojiwa mara tu alipowasili nchini humo.

Hata hivyo, Msemaji wa Interpol aliyekataa kutaja jina lake, aligoma kusema kama Hongwei alikwenda China kwa kazi maalum. Taarifa zinadai kuwa Hongwei alikwenda nchini humo kuichokonoa Beijing.

Katika hatua nyingine, Wizara ya Mambo ya Ndani nchini Ufaransa hapo jana ilitoa ripoti ya kwamba, mke wa Hongwei alikwenda katika makao makuu ya Interpol yaliyoko mjini Lyon nchini humo, kuripoti taarifa za kupotea kwa mume wake.

Taarifa ya wizara hiyo, ilieleza kuwa, Ufaransa inafanya uchunguzi wa tukio hilo ambapo imefungua jalada la uchunguzi,  vile vile  linafuatilia vitisho anavyopokea mke wa rais huyo, sambamba na polisi wake kutumia mbinu za hali ya juu kuhakikisha mwanamama huyo anakuwa salama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Chadema: Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

error: Content is protected !!