Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko China kuchangia 98 Bil. ujenzi makao makuu ya ulinzi Dodoma
Habari Mchanganyiko

China kuchangia 98 Bil. ujenzi makao makuu ya ulinzi Dodoma

Venance Mabeyo, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania
Spread the love

SERIKALI ya China imepanga kutoa Yuan RMB 300 Milioni (Tsh. 98,084,910,435.8), kwa ajili ya kuimarisha ulinzi nchini ikiwemo, ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa, jijini Dodoma. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Hayo amesema Jenerali Venance Mabeyo, Mkuu wa Majeshi nchini, leo tarehe 25 Novemba 2019 katika hafla ya uwekaji jiwe la msingi la ujenzi wa makao makuu hayo, iliyofanyika Kikombo, Wilaya ya Chamwino jijini Dodoma.

Jenerali Mabeyo amesema sehemu ya fedha hizo zitatumika kujenga makao makuu yanayokidhi viwango vya kimataifa, ambapo kutakuwa na  ofisi maalumu ya Amiri Jeshi Mkuu wa Nchi, kwa ajili ya kutekeleza majukumu yake ya ulinzi wa taifa.

Mkuu huyo wa Majeshi amesema China imetenga fedha hizo, baada ya Tanzania kuiomba msaada wa kuboresha dhana za jeshi na ujenzi wa makao makuu hayo.

“Ombi la tatu kwa China ilikuwa ni ujenzi wa eneo hili la makao makuu, yanayokidhi viwango vya kimataifa. Kwa maana kwamba, Amiri Jeshi Mkuu anaweza akafanyia kazi hapa, akatekeleza majukumu ya kiulinzi akiwa katika makao makuu ya kiulinzi,” amesema  Jenerali Mabeyo na kuongeza;

“Kwa maana unakuwa na ofisi maalumu hapa, ya kutoa maekelezo ya kiulinzi. Naomba nikufahamishe kwamba, marafiki zetu walikubali na kwa sasa hivi tayari wametenga RMB 300 milioni.”

Wakati huo huo, Jenerali Mabeyo amempongeza Rais John Magufuli kwa kuafiki ujenzi wa makao makuu hayo, pamoja na juhudi zake katika kuimarisha utendaji kazi wa majeshi nchini, pamoja na kuboresha maslahi ya askari wa jeshi.

Jenerali Mabeyo amesema Jeshi linamuunga mkono kwa hatua anazochukua.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari Mchanganyiko

GGML yasisitiza kuendelea kuimarisha afya za wafanyakazi

Spread the loveKAMPUNI ya Geita Gold Mining Limited kwa kushirikiana na kampuni...

error: Content is protected !!