CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kinaweza kukimbiwa na viongozi wake wengine watatu, wakiwamo wabunge wawili wa majimbo, anaandika Mwandishi Wetu.
Taarifa kutoka ndani ya chama hicho na Ikulu jijini Dar es Salaam zinasema, mkakati mkali unasukwa wa kuwashawishi viongozi hao kukihama chama hicho na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Hata hivyo, mmoja wa viongozi anayeshawishiwa kuondoka amenukuliwa akisema, hajafikiria kufanya hivyo na kwamba hata ikimbidi kuondoka ndani ya Chadema, hatajiunga na CCM, bali atafanya shughuli zake binafsi.
Kupatikana kwa taarifa hizi kumekuja muda mchache baaada ya mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Pastrobas Katambi kujiunga na CCM leo Ikulu jijini Dar es Salaam.
Aidha, kupatikana kwa taarifa hizi kumekuja wiki tatu baada ya gazeti hili kuripoti kuwapo kwa mpango wa wabunge wa viongozi wa Chadema kukima chama hicho.
Hakuna kitu apo, hata angehama Mbowe bado CDM Haitakufa watu wenye akili timamu ndi wanakuja kama Mhe Nyalandu, hatuangalii mtu na utashi wake kama patrobas ameshindwa kuitumikia nafasi yake njia iko wazi watakuja wengine.Hata kwenye kanisa watu wanaokoka na kurudi nyuma sembuse siasaAMERUDI KWENYE MATAPUTAPU HUYU, AMERUDIA MATAPISHI YAKE MWENYEWE