Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yaanza kumsulubu Nyalandu
Habari za SiasaTangulizi

Chadema yaanza kumsulubu Nyalandu

Lazaro Nyalandu, aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii. Picha ndogo waziri wa sasa wa wizara hiyo, Dk. Hamisi Kigwangalla
Spread the love

SIKU chache baada ya aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu kujivua uanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na nafasi yake ya ubunge na kujiunga na Chadema, ameanza kuonja chungu ya uamuzi wake, baada kushutumiwa kwa matumizi mabaya ya madaraka, anaandika Dany Tibason.

Shutuma hizo dhidi ya Nyalandu zimeibuliwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamis Kigwangalla bungeni leo alipokuwa akichangia Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa mwaka 207/2018.

Dk Kigwangalla ameiagiza Takukuru na polisi kumchunguza Nyalandu kwa matumizi mabaya ya madaraka ili sheria ichukue mkondo wake.

Waziri huyo amesema Nyalandu alipokuwa waziri aliikosesha serikali mapato ya Sh. 32 bilioni kwa miaka miwili aliyohudumu katika wizara hiyo kwa kushindwa kusaini sheria ya tozo kwa hoteli za kitalii.

Mbali na tuhuma hiyo, pia alimtuhumu kutumia helkopta ya mwekezaji mmoja raia wa kigeni, kipindi cha kampeni zake za kugombea urais 2015, wakati kampuni ya raia huyo ilikuwa ikituhumiwa kwa ujangili.

Nyalandu aliwahi kuliliwa akisema kuwa tuhuma ambazo zimeanza kuibuliwa mitandao dhidi yake si za kweli bali zinalenga tu kumchafua na kuhoji iweje ziibuliwe sasa zaidi ya miaka miwili tangu aachie uwaziri.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!