Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema wateua wa kupambana na Waitara, Kalanga
Habari za Siasa

Chadema wateua wa kupambana na Waitara, Kalanga

Spread the love

CHAMA cha Chadema kimeteua wagombea ubunge katika majimbo matatu yaliyoachwa wazi baada ya wabunge wawili kujiuzulu na mmoja kufariki. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Uteuzi huo umefanywa leo tarehe 17 Agosti, 2018 na Kamati Kuu ya Chadema na kutangazwa na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano Chadema, Tumaini Makene.

Kamati hiyo iliyoketi kwa muda wa siku mbili, imemteua Asia Msangi kuwa mgombea kwenye Jimbo la Ukonga, Yonas Laiser amechaguliwa kukiwakilisha chama hicho katika jimbo la Monduli na Amina Saguti ameteuliwa kugombea Korogwe Vijijini.

Katika majimbo hayo, mawili yalikuwa yanashikiliwa na makada wa Chadema akiwemo Mwita Waitara (Ukonga) na Julius Kalanga (Monduli) ambao hivi karibuni walijivua uanachama wa chama hicho na kujiuzulu ubunge.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

error: Content is protected !!