Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema wamvimbia Spika Ndugai
Habari za Siasa

Chadema wamvimbia Spika Ndugai

Job Ndugai, aliyekuwa Spika wa Bunge Tanzania
Spread the love

WABUNGE wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wameagizwa kutotii agizo la Job Ndugai, Spika wa Bunge kwamba warejeshe fedha za posho walizopewa. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea).

John Mnyika, Katibu Mkuu wa Chadema amesema, Kati Kuu ya chama hicho imetafakari na kuona kuwa, hakuna sababu ya wabunge hao kurejesha fedha hizo kama ilivyoamriwa na mahakama.

Tarehe 6 Mei 2020, Spika Ndugai aliwataka wabunge wa Chadema waliogoma kuhudhuria vikao vya bunge kwa kujiweka karantini, warejeshe fedha za posho walikopewa za Bunge.

Akisistiza agizo hilo Spika Ndugali alisema, endapo mbunge atakaidi agizo hilo, itamlazimu atakaporejea awe na cheti kinachoonesha amepima ugonjwa wa corona na majibu yake ama hatua zaidi zitachukuliwa.

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 11 Mei 2020, wakati akieleza maazimio ya Kamati Kuu ya chama hicho, Mnyika amesema “Kamati Kuu imeagiza wabunge kutotekeleza maagizo hayo, kwa kuwa ni kinyume cha sheria.”

Amesema, Kamati Kuu kuu imejiridhisha kuwa wabunge wake wake si wezi na kwamba, fedha hizo hawajaiba hivyo hawana sababu ya kuzirejesha.

“Azimio la sita ni juu ya madai yaliyotolewa na Spika Ndugai, kwamba wabunge wa Chadema waliopewa posho za kujikimu za kuishi Dodoma ni wezi.

“Kamati imefikia uamuzi, kwamba madai haya ya spika ni ya uongo na kutoa rai kwa wabunge kutokutekeleza yale ambayo spika ameleekeza kinyume na Katiba na sheria za nchi,” amesema Mnyika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!