Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema waishtaki Serikali ya JPM Umoja wa Ulaya
Habari za SiasaTangulizi

Chadema waishtaki Serikali ya JPM Umoja wa Ulaya

Wabunge na Madiwani wa Chadema wakiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wa Umoja wa Ulaya
Spread the love

WABUNGE na Madiwani wa Chama cha Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wameishitaki SErikali ya Tanzania kwa Umoja wa Ulaya juu ya hali ya kisiasa na kushinikiza kupatiwa dhamana viongozi wa chama hicho pamoja na kutahadhalisha usalama wa viongozi hao. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Viongozi hao waliongozwa na Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbles Lema, Peter Lijualikali, Mbunge wa Kilombero, Joseph Haule mbunge wa Mikumi. Wengine ni Boniface Jacob, Meya wa Ubungo, Patrick Ole Sosopi, Mwenyekiti wa Bavicha na wengine zaidi ya 30.

Viongozi wa chama hicho walikosa dhamana Machi 27, 2018 baada ya viongozi serikali kuzuia dhamana zao.
Lema aliyeongoza msafara huo alisema kuwa wataomba hati tahadhari kwenye ubalozi huo.

Amesema kuwa chama hicho kitawaomba ubalozi huo kusiishie tu kutoa matamko ya kupinga kinachoendelea nchini bali waende mbele zaidi na kwa kuchukua hatua stahiki.

Wabunge na Madiwani wa Chadema wakiwa katika mkutano na Ubalozi wa Umoja wa Ulaya
Wabunge na Madiwani wa Chadema wakiwa katika mkutano na Ubalozi wa Umoja wa Ulaya

Lema amesema kushikiliwa kwa viongozi wao kunatoa tafsiri kuwa chama chote kimefungwa gerezani licha kuwepo mkakati wa serikali kukifunga chama hicho.

Wakati Wabunge na Madiwani wa Chadema wakiwa Ubalozi wa Umoja wa Ulaya, kesi ya viongozi wao inaendelea Makahama ya Kisutu bila ya watuhumiwa kufikishwa mahakamani hapo.

Hakimu Mkazi, Wilbard Mashauri anasikiliza kesi hiyo na kutoa uamuzi wake juu ya dhamana yao. MwanaHALISI Online itawajuza kinachoendelea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!