Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema waipa serikali fikra mpya
Habari za Siasa

Chadema waipa serikali fikra mpya

Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Pwani, kimeitaka serikali kuubinafsisha Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka Dar es Salaam, ili kuongeza ufanisi katika utoaji huduma. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Wito huo umetolewa leo tarehe 30 Desemba 2019 na Baraka Mwago, Makamu Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani.

Mwago ameeleza kuwa, huduma zinazotolewa na mradi huo hazikidhi kiwango, na kusababisha usumbufu kwa wananchi.

Miongoni mwa adha wanayokumbana nayo watumiaji wa mradi huo, ni msongamano wa abiria vituoni na kwenye gari.

“Huu mradi wenzetu hawajajipanga. Mwendokasi wanasema wana magari 200 yamekwama bandarini lalini wanapishana na serikali kulipa kodi. Serikali ibinafsishe mradi wa mwendokasi ili wananchi wapate huduma bora,” ameshauri Mwago.

Wakati huo huo, Mwago ameishauri Serikali kukarabati miundombinu ya Jiji la Dar es Salaam, ili kuondoa changamoto ya mafuriko katika jiji hilo.

Badala ya miradi hii mikubwa ambayo haina faida, fedha hii ingetumika kuikarabati miuondombinu ya Dar es Salaam. Kuboresha mifereji inayoelekea kwenye mto au baharini,” amesema Mwago.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!