Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema wabuni njia mpya kumkabili Rais Magufuli
Habari za Siasa

Chadema wabuni njia mpya kumkabili Rais Magufuli

John Mnyika, Mbunge wa Kibamba(wakwanza) na Boniface Jacob, Meya wa Ubungo
Spread the love

JOHN Mnyika, Naibu katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Kibamba amesema kuwa rais Magufuli anatumia kivuli cha kuleta maendeleo kuminya demokrasia nchini, anaandika Hellen Sisya.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo la Kimara Mwisho jimboni humo,mbunge huyo amesisitiza kuwa demokrasia na maendeleo ni lazima viende pamoja.

“Rais Magufuli anataka kwa kivuli cha kuleta maendeleo, serikali isikosolewe pale inapokosea kuhusu maendeleo, kwa kuminya demokrasia, na sisi tunasema demokrasia na maendeleo ni lazima viende pamoja” alisema mbunge huyo.

Aidha, Mnyika aliongeza kuwa chama chake kitatumia mikutano ya kiserikali inayofanywa na wabunge pamoja na madiwani wake kufanya shughuli za chama kama ambavyo Rais Magufuli anatumia mikutano ya kiserikali kushughulika na kazi za chama chake.

“Kwa sababu rais Magufuli ameingia madarakani, amekataza mikutano ya vyama. Na anatumia mikutano ya kiserikali kushughulika na mambo ya CCM. Na sisi pia tumefikia uamuzi kwamba katika mikutano yetu yote ya hadhara, tutashughulika na masuala ya maendeleo, lakini pia tutashughulika na masuala ya demokrasia ” ,alisisitiza Mnyika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!