Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Chadema Morogoro  waangusha maombi kwa Lissu
Habari Mchanganyiko

Chadema Morogoro  waangusha maombi kwa Lissu

Tundu Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki, akilia kwa uchungu
Spread the love

UONGOZI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kanda ya kati pamoja na uongozi wa Chadema mkoa wa Morogoro wameungana kufanya maombi ya kumwombea mbunge wa Singida Mashariki ,  Tundu Lissu pamoja na kuhamasisha michango kwa ajili ya matibabu.

Maombi hayo  yalifanywa na uongozi wa kanda ya  kati pamoja na uongozi wa Chadema mkoa wa Morogoro   huku wakilaani  vitendo vya  polisi kuendelea  kuwakamata na kuwanyanyasa wapinzani.

Viongozi hao wa Chadema wamesema polisi wameshindwa kuwakamata ama kutoa taarifa za watu ambao wanafanya uhalifu lakini hawabainiki.

Awali viongozi hao wa chadema kanda ya kati pamoja na mkoa Morogoro walikutana kwa lengo la kuweka uongozi wa Chadema msingi ambao utafanya kazi ya kuratibu shughuli zote za kuimarisha chama ikiwa ni pamoja na kukijenga.

Akifungua kikao hicho mwenyekiti wa Chadema kanda ya kati,  Alphonce Mbassa amesema kuwa licha ya kuwepo changamoto kubwa ya kufanya siasa kwa sasa kutokana na serikali kwa kutumia vyombo vya dola kuukandamiza upinzania, lakini ni lazima chama kiweke mikakati ya kuimarisha.

Akizungumzia kuhusu suala la  polisi kuwakamata viongozi wakiwa katika shughuli zao za kawaida,  Mbassa amesema umefika wakati wa wanachama kutambua kwamba wanatakiwa kutumia nafasi zao kufanya siasa bila kuwa na uoga.

“Nataka niwaeleze viongozi na wapenzi wa Chadema kanda ya kati, mkoa wa Morogoro pamoja na taifa kwa ujumla, wote mnajua kuwa kiongozi wetu Tundu Lissu alipigwa risasi,  lakini imekuwa shida sana kuandaa maombi, kuvaa tishert ni shida hata kufanya  michango imeoneekana kuwa ni jambo la kisiasa.

“Mkiona hali kama hiyo sasa hapo ndo pakujua kuwa serikali inaelekea kuanguka na vyama vya upinzani kuchukua dola” amesem Mbassa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!