Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema kuwafuta machozi watumishi wa umma
Habari za Siasa

Chadema kuwafuta machozi watumishi wa umma

Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) nchini Tanzania kimeahidi kulipa malimbikizo ya madeni ya watumishi wa umma pamoja na kuwaongezea mishahara. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbulu … (endelea).

Ahadi hiyo imetolewa jana Jumatano tarehe 16 Septemba 2020 na Mgombea mwenza wa urais wa Tanzania wa Chadema, Salum Mwalimu wakati akizungumza katika kampeni chauchaguzi huo wilayani Mbulu Mkoa wa Manyara.

Mwalimu alisema, Chadema kikifanikiwa kushinda uchaguzi huo, Serikali yake itapeleka bajeti ya nyongeza bungeni kwa ajili ya kuongeza mishahara ya watumishi wa umma na kuwapandisha madaraja.

Akikazia hoja hiyo, Mwalimu alisema, Serikali ya Chadema italipa fedha za watumishi wote wa umma waliohamishwa vituo vya kazi bila kulipwa stahiki zao.

“Tunafahamu kuna watumishi wa umma waliohamishwa vituo vya kazi bila kupewa stahiki zao, Chadema tunasema tutahakikisha kila mtumishi wa umma aliyehamishwa na hakupewa stahiki zake tunakwenda kulipa,” amesema Mwalimu.

Salimu Mwalimu ni mgombea Mwenza wa Tundu Lissu, ambaye amepewa ridhaa ya Chadema kupeperusha bendera yake katika uchaguzi wa kiti cha Urais wa Tanzania.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!