Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CCM wafurika kuchukua fomu za Ubunge Moshi Mjini
Habari za Siasa

CCM wafurika kuchukua fomu za Ubunge Moshi Mjini

Mkurugenzi wa Ibraline Foundation , Ibrahim Shayo akiingia kwenye gari mara baada ya kuchukua fomu ya kugombea ubunge jimbo la Moshi mjini katika ofisi za Chama cha Mapinduzi(CCM)
Spread the love

MAKADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jimbo la Moshi Mjini wamefurika kwenye ofisi ya chama hicho wilaya kuchukua fomu za kuomba kuteuliwa kugombea ubunge. Anaandika Mwandishi Wetu, Kilimanjaro…(endelea).

Leo tarehe 14 Julai 2020, ni siku ya kwanza kwa watia nia wa CCM kuchukua fomu za kuomba kupitishwa na chama hicho, zoezi hilo linatarajiwa kuhitimishwa tarehe 17 Julai 2020.

Mpaka kufika saa 8 mchana wa leo, jumla ya makada saba walikuwa tayari wamechukua fomu huku taarifa zikieleza, wengine wapo njiani kujitokeza.

Waliochukua fomu mpaka sasa ni Mkurugenzi wa Ibraline Foundation na Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa Mkoa wa Kilimanjaro, Ibrahim Shayo.

Wengine ni Priscus Tarimo, Issah Wilium, Noel Nko, Mwalimu Evans Mghase, Faraji Swai na Alfa Kiwango. Kwa leo, zoezi hilo linatarajiwa kuhitimishwa saa 12:00 jioni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!