Thursday , 25 April 2024
Habari za Siasa

CCM wabanana mbavu

Mizengo Pinda, Waziri Mkuu Mstaafu
Spread the love

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Iringa kimetengeneza utaratibu mpya wa kuwapima madiwani na wabunge wake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Iringa … (endelea).

Sasa mbunge na diwani kwenye mkoa huo, atatakiwa kukutana na wananchi kila baada ya miezi mitatu na kueleza nini amefanya kwenye kipindi hicho.

Uamuzi huo umefikiwa kwenye kikao maalumu cha chama hicho kilichowakutanisha wabunge na madiwani hao ambapo Dk. Abel Nyamahanga, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa amesema “itasaidia kufuatilia ahadi zao.”

Dk. Nyamahanga amesema, chama hichi kimeweka utaratibu huo kuwalazimisha viongozi hao kutoa taarifa lakini pia kuonesha mafanikio ya uchapaji kazi wao.

Amesema, hatua hiyo pia itaongeza imani ya wananchi kwa CCM na kurahisisha uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kwa chama hicho.

Kikao hichi pia kimehudhuriwa na Mizengo Pinda, Waziri Mkuu Mstaafu ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa.

Pinda amewataka wabunge na madiwani hao kuwa karbu na wananchi ili kujua changamoto zinaqzowakabilia na kujua namna ya kuzitatua.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!