Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CCM kumweka kikaangoni Mwita Waitara
Habari za SiasaTangulizi

CCM kumweka kikaangoni Mwita Waitara

Mwita Waitara
Spread the love

CHAMA cha Mapinduzi (CCM) Mkoani Mara kimesema kitamuita kwenye Kamati ya Maadili, Mwita Waitara, Naibu Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI, ili kujibu tuhuma za kuvunja kanuni za uchaguzi za chama hicho. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Akizungumza na Wanahabari jana tarehe 3 Januari 2020, Samweli Kiboye, Mwenyekiti wa CCM Mkoani Mara, amesema Waitara amefanya makosa kujinadi kuwa atagombea Jimbo la Tarime Vijijini,  kinyume na katiba ya chama hicho, kwa kuwa kipindi cha uchaguzi bado hakijafika.

“Lazima tutumie kanuni zetu za CCM,  kanuni za uchaguzi, lazima tumwite katika vikao vyetu hatuwezi kumuacha mtu anajinadi. Kwa sababu akishaanza kujinadi ataleta makundi Tarime, tunataka WanaTarime tuikomboe Tarime, tunavyoenda hivi tutaleta makundi,” amesema Kiboye.

Mwenyekiti huyo wa CCM mkoani Mara, amesema Mwita ataitwa kwenye kamati hiyo, ili kujibu utaratibu aliotumia kujitangaza kugombea Ubunge wa Tarime Vijijini.

“Atatueleza ametoa mfumo wake wapi wa kujitangaza, au kama yeye anajiona yuko juu ya chama ndani ya Tarime, asije akatuharibia chama Wilaya ya Tarime,” ameeleza Kiboye.

Kiboye ameonya watu wanaoanza kujinadi kugombea katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, akisema kwamba, hatamuogopa mtu yeyote kwa kuwa hakuna mtu aliye juu ya CCM.

“Natoa onyo vikao vitafuata na hatutamuonea mtu haya, hatutamuogopa yeyote awe na cheo kiasi gani, chama ndio kikubwa. Hakuna mtu aliyejuu ya chama, chama ndio bosi uhoji mtu yeyote, lazima tuwahoji tutawaita katika kamati ya maadili,” ameonya Kiboye.

Mwita ambaye ni Mbunge wa Ukonga, hivi karibuni alitangaza kugombea ubunge wa jimbo hilo, na kuahidi kuchuana na John Heche, Mbunge wa Tarime Vijijini, kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari MchanganyikoTangulizi

Baba aomba msaada kuzika miili ya familia yake iliyofunga bila kula kuonana na Mungu

Spread the loveWAKATI Mamlaka nchini Kenya, ikiendelea kukabidhi miili ya watu waliofariki...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

error: Content is protected !!