SELEIMAN Said Bungara maarufu Bwege, amengushwa ubunge wa Kilwa Kusini kupitia ACT-Wazalendo katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarege 28 Oktoba 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Wetu…(endelea)
Bwege ambaye amekuwa maarufu ndani na nje ya Bunge kutokana na aina yake ya kuzungumza au kuchangia mijadala bungeni, ameangushwa na mgombea wa CCM, Kassinge Ally.
Hivi karibuni Bwege akitumia msemo wa ‘ulisikia wapi’ aliingia bungeni kwa mara ya kwanza mwaka 2010 kupitia Chama Cha Wananchi (CUF).
Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 201 5, wananchi wa Kilwa Kusini waliendelea kumwamini Bwege aliyezaliwa Novemba 18 mwaka 1961 kwa kumrejesha bungeni kuendelea kuwawakilisha.
Bwege alikihama chama chake cha CUF na kujiunga na ACT-Wazalendo na kupitishwa kuwania ubunge jimboni himo lakini amejikuta akishindwa.
Leave a comment