Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge: Wadaiwa matrekta ya SUMA JKT wabanwe
Habari za Siasa

Bunge: Wadaiwa matrekta ya SUMA JKT wabanwe

Matrekta yakiwa katika ofisi za SUMA JKT Mwenge
Spread the love

SERIKALI inatakiwa kuchukua hatua dhidi ya wanasiasa wakiwemo wale waliostaafu ambao wameshindwa kurejesha mikopo ya matrekta waliyopata kutoka Shirika la Uzalishaji Mali linaloendeshwa na Jeshi la Kujenga Taifa (SUMA JKT). Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Agizo hilo limetolewa bungeni na mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Naghenjwa Kaboyoka wakati akiwasilisha taarifa ya kazi za kamati hiyo kwa mwaka wa 2018.

Kaboyoka ambaye ni mbunge kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), alisema kuna limbikizo kubwa la deni linalotokana na hatua ya kutorejeshwa mikopo ambayo kwa sehemu kubwa walionufaika ni wanasiasa.

Wanufaikaji wengine wa mikopo hiyo iliyofikia thamani ya Sh. Bilioni 40 na ambayo ilianza kutolewa mwaka 2011 mpaka 2016, ni taasisi mbalimbali. Taarifa ya Kaboyoka ilisema deni hilo ni la kufikia Juni 30 mwaka 2017.

Alisema uchambuzi wa kamati umebaini kuwa baadhi ya wadaiwa sugu wa mikopo ni viongozi katika serikali wa sasa na waliostaafu.

“Kama jitihada za dhati hazitafanyika kuna viashiria kuwa madeni hayo hayatalipwa na kuiweka Suma JKT katika hali ngumu kiutendaji… kutorejesha mikopo ni ukiukaji wa mikataba na ni kuisababishia hasara serikali,” alisema.

Ndipo alipotoa kauli kwamba, “… Bunge linaazimia kwamba serikali ifanye uchunguzi wa kina ili kubaini taratibu zilizotumika katika utoaji wa mikopo ya matrekta kwa watu na taasisi mbalimbali na ichukue hatua stahiki kwa wahusika wanaodaiwa.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Deni la Serikali laongezeka kwa trilioni 11

Spread the loveDENI la Serikali imeongezeka kwa takribani Sh. 11 trilioni sawa...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

error: Content is protected !!