Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge limepoteza sifa yake-Mngwali
Habari za Siasa

Bunge limepoteza sifa yake-Mngwali

Jengo la Bunge la Tanzania mjini Dodoma
Spread the love

RIZIKI Shahari Mngwali, Mbunge wa Mafia- viti maalum kwa tiketi ya Chama cha Wananchi- CUF amesema Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepoteza sifa yake, anaandika Pendo Omary.

Amesema kupoteza sifa kwa Bunge kunatokana na Bunge lenyewe kukosa hadhi ya kuwa mhimili unaojitegemea badala yake kufanya kazi kama wakala wa serikali.

Riziki ambaye ni kiongozi wa wabunge wa CUF bungeni amesema “niliingia bungeni kwa hamu kweli. Nikidhani ni chombo kikubwa kinachowakilisha wananchi na kinachofanya maamuzi kwa kujitegemea lakini nimekatishwa tamaa.”

“Nilitarajia sisi ni wawakilishi wa wananchi na msimamizi wa serikali. Yale mamlaka ya kikatiba ya Bunge siyaoni katika bunge hili. Mfano sisi wabunge wa upinzania tunavyoihoji serikali au kuishauri mara nyingi kiti cha spika au wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanatumika kuitetea. Sio wajibu wao,” anaeleza Riziki.

Mbali na Bunge kutumiaka kama wakala wa serikali, Riziki amesema mbunge mmoja mmoja hapewi hadhi inayotakiwa kama mwakilishi wa mamilioni ya wananchi badala yake hata hukumu dhidi yake zinatolewa kama mtu binafsi.

Soma mahojiano zaidi katika gazeti la MwanaHALISI la Jumatatu wiki ijayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!