Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge kuhitimishwa Juni 16, Bajeti kujadiliwa siku mbili
Habari za Siasa

Bunge kuhitimishwa Juni 16, Bajeti kujadiliwa siku mbili

Bunge la Tanzania
Spread the love

BUNGE la 11 la Tanzania linaloongozwa na Spika Job Ndugai, litahitimishwa Jumanne ijayo tarehe 16 Juni 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Ratiba iliyotolewa leo Jumatano tarehe 10 Juni 2020 na Ofisi ya Bunge la Tanzania inaonyesha, Rais wa Tanzania, John Magufuli, atahutubia Bunge hilo Jumanne ijayo saa 3 asubuhi.

Awali, ratiba ilikuwa ikionyesha Bunge hilo ambalo Rais Magufuli alilizindua tarehe 20 Novemba 2015, lingehitimishwa tarehe 19 Juni 2020.

Katika ratiba hiyo mpya, kesho Alhamisi tarehe 11 Juni 2020 itawasilishwa taarifa ya hali ya uchumi na Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2020/2021.

Ijumaa na Jumamosi tarehe 12 na 13 Juni 2020 itakuwa ni mjadala kuhusu taarifa ya hali ya uchumi na bajeti ya serikali huku Jumatatu ya tarehe 15 Juni 2020 itahitimishwa.

Mjadala wa bajeti hiyo itajadiliwa kwa siku mbili ikiwa ni tofauti na miaka ya nyuma ambapo bajeti ilikuwa ikijadiliwa kwa siku saba.

Jumatatu hiyo hiyo ya tarehe 15 Juni 2020, Bunge litapiga kura ya Bajeti ya Serikali, Kujadili Muswada wa Sheria ya Fedha za Matumizi wa Mwaka 2020 (The Appropriation Bill, 2020) (hatua zote).

Pia, kujadili Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka,2020(TheFinanceBill,2020) ( kusomwa mara ya pili, Kamati ya Bunge zima na kusomwa mara ya tatu] kasha Bunge hilo litapitisha Azimio la Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kanuni kuhusu Marekebisho ya Kanuni za Bunge.

Siku hiyo, itahitimishwa kwa Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa kutoa hotuba yake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!