Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bulembo atangaza kung’atuka CCM
Habari za Siasa

Bulembo atangaza kung’atuka CCM

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi la Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdallah Bulembo
Spread the love

ALHAJI Abdallah Bulembo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), ametangaza kung’atuka rasmi katika nafasi yake, kwa mdai kuwa anahitaji kuumzika, anaandika Dany Tibson.

Bulembo ambaye hivi karibuni ameteuliwa kuwa Mbunge na Rais John Magufuli amesema hana mpango wa kugombea nafasi yoyote ndani ya CCM katika uchaguzi mkuu wa chama hicho unaofanyika mwaka huu.

Ametoa kauli hiyo katika baraza la dharura la jumuiya ya wazazi wa CCM kilichohudhuriwa na wajumbe 102.

“Si kwamba sina uwezo wa kugombea tena, ila tu nimeamua kupumzika na nikatulie kijiji  kwangu huku nikiendeleza shughuli nyingine.

“Msidhani kwamba nang’atuka kutokana na ubunge niliochaguliwa. Hapana, mimi ni mbunge ambaye jimbo langu ni Ikulu,” amesema.

Amesema ni wakati wa wajumbe wengine kutoka ndani ya jumuiya hiyo kuchangamkia fursa ya kugombea nafasi hiyo ya uwenyekiti bila kutegemea kubebwa na mtu yoyote.

“Msitegemee kuwa nitampigia mtu kampeni, nendeni mkachukue fomu ya kugombea kama mmejipima na kuona mna uwezo na asije mtu yoyote akasikika huko akiwadanganya kuwa ameongea na mimi na kwamba nitamuunga mkono katika uchaguzi,” amesisitiza.

Bulembo amedai kuwa mwanzoni Jumuiya ya wazazi ya CCM ilikuwa na wakati mgumu lakini yeye kama mwenyekiti kwa kushirikiana na viongozi wengine waliamua kufanya kazi ya kuiweka mahali mazuri jumuiya hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!