Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bulaya, Mdee wazuiwa kuingia bungeni mpaka mwakani
Habari za SiasaTangulizi

Bulaya, Mdee wazuiwa kuingia bungeni mpaka mwakani

Wabunge Ester Bulaya na Halima Mdee
Spread the love

BUNGE la Tanzania limetoa hukumu kwa Wabunge Halima Mdee wa Kawe na Esther Bulaya wa Bunda kutohudhuria vikao vyote vya bunge vinavyoendelea mpaka mkutano ujao wa Bunge la Bajeti ya 2018/19, anaandika Hamisi Mguta.

Kamati ya Maadili  leo imesema Bulaya na Mdee wamemaliza adhabu za kawaida zilizopo kwenye kanuni za bunge, huku hukumu hiyo ikiungwa mkono na wabunge wengi.

Hata hivyo, Bunge liliendelea  kujadili makosa ya wabunge hao huku George Mkuchika, Mwenyekiti wa kamati hiyo akiomba Bunge kujadili adhabu inayostahili kulingana na makosa yao.

Kanuni inasema, mbunge anayefanya kosa la kwanza anaweza akazuiwa kuhudhuria vikao visivyozidi 10 na atayakosea kwa mara ya pili anaweza kuzuiwa kuhudhuria vikao visivyozidi 20.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!