Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Michezo Bosi GSM kuongoza kamati ya ushindi Taifa Stars
Michezo

Bosi GSM kuongoza kamati ya ushindi Taifa Stars

Ghalib Said Mohammed
Spread the love

RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia amemteuwa Ghalib Said Mohammed kuwa Mwenyekiti wa kamati ya ushindi ya Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kuelekea mchezo wa kufuzu AFCON dhidi ya Tunisia. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea). 

Ghalib ambaye ni mkurugenzi wa kampuni ya GSM ambao ni wafadhili wa kuu wa klabu ya Yanga ataongoza kamati hiyo ambayo ina wajumbe 13. 

Viongozi wengine wa kamati wa kamati hiyo ni Salim Abdallah ‘Try Again’ ambaye ni makamu mwenyekiti, huku katibu wa kamati hiyo ni Mhandisi Hersi Said ambaye ni mjumbe wa mashindano klabu ya Yanga.

Salim Abdallah ‘Try Again’

Wajumbe walioteuliwa kwenye kamati hiyo ni Abdallah bin kleb, Haji Manara, Jerry Muro, Patrick Kahemele, Zacharia Hanspope, Beatrice Singano, Christina Manyenye, Said Nassor.

Wengine ni Anitha Rwehumbiza, Farid Nahdi, Feisal Abri, Farough Baghozal, Nandi Mwinyimbella na Phelomen Ntahijala.

Taifa Stars inatarajia kucheza mchezo wa kufuzu Kombe la Mataifa Africa, AFCON dhidi ya Tunisia utakaopigwa 13 Novemba, 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Ujanja ni kubeti na Meridianbet

Spread the love  JUMAPILI ya leo imekaa kihela hela sana ndani ya...

Michezo

Anza Jumamosi yako na mkwanja wa Meridianbet

Spread the loveJumamosi ya leo ODDS zimekaa kijanja sana ndani ya Meridianbet...

error: Content is protected !!