Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Bosco Ntaganda akutwa na hatia
Kimataifa

Bosco Ntaganda akutwa na hatia

Bosco Ntaganda
Spread the love

MAHAKAMA ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC), imemtia hatiani kwa makosa ya uhalifu wa kivita na binadamu Bosco Ntaganda,  kiongozi wa zamani wa waasi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Majaji wa ICC wamemkuta na hatia Ntaganda kwa makosa 18 ya uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu, uliotokea katika Mji wa Mashariki wa Ituri mwaka 2002 na 2003.

Robert Fremr, Jaji wa ICC amesema, Ntaganda anatuhumiwa kutoa amri zenye lengo la kuuwa na kutesa raia wasio na hatia, alipokuwa kiongozi wa waasi.

Makosa mengine yaliyotajwa na waendesha mashtaka hao ni pamoja na kuhusishwa na vitendo vya ubakaji na utumwa wa ngono, kumuuwa kasisi wa kikatoliki pamoja na kuwasajili watoto kwenye jeshi wakiwemo wasichana.

Vile vile, Ntaganda anatuhumiwa kuongoza operesheni ya waasi wa Union of Congolese Patriots (UCP).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!