Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Bodi ya Mikopo kukopesha wanachuo 128,285
ElimuHabari za Siasa

Bodi ya Mikopo kukopesha wanachuo 128,285

Bodi ya Mikopo Elimu ya Juu
Spread the love

BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), inatarajiwa kutoa mikopo kwa wanafunzi 128,285 sawa na ongezeko la asilimia 4.5 ikilinganishwa na mwaka wa fedha uliopita (2018/19). Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Kati yao, wanafunzi 45,485 watakuwa wa mwaka wa kwanza ikiwa ni ongezeko la silimia 10.3 ikilinganishwa na wanafunzi 41,234 wa mwaka 2018/19.

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 29 Aprili 2019 bungeni na Prof. Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia wakati akiwasilisha bungeni Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2019/2020.

Prof Ndalichako amesema kuwa, bodi hiyo itafuatilia fedha inayolipwa ili kuhakikisha fedha za mikopo zinawafikia kwa wakati wanafunzi stahiki.

Amesema, bodi hiyo imepanga kutekeleza mambo kadhaa ambayo ni kutoa mikopo yenye thamani ya Sh, 450 Bil ambapo ni ongezeko la asilimia 5.0 ikilinganishwa na mwaka 2018/19.

“Kukusanya Sh. 221.5 Bil kutoka kwa wanufaika ambao mikopo yaio imeiva, hili ni ongezeko la asilimia 40.5 ukilinganuisha na lengo la mwaka 2018/19 ambalo ni Sh. 157.7 Bil,” amesema.

Prof. Ndalichako amesema, HESLB itaanzisha na kuimarisha ofisi mbili za kanda katika Mikoa ya  Mbeya na Mtwara ili kufikisha jumla ya ofisi sita za kanda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!