Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Bodi mpya NCAA yaahidi kutatua changamoto
Habari Mchanganyiko

Bodi mpya NCAA yaahidi kutatua changamoto

Kaimu Mwenyekiti mpya wa bodi ya NCAA, Mudhihir Mudhihir
Spread the love

BODI ya Mamlaka ya Ngorongoro (NCAA), imesema itakabiliana na changamoto zinazoikabili mamlaka hiyo kufikia dira ya uhifadhi, anaandika Mwandishi Wetu.

Kaimu Mwenyekiti mpya wa bodi hiyo, Mudhihir Mudhihir, amesema hayo juzi baada ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe kuizindua jijini hapa.

Amesema wajumbe wa bodi hiyo ambao ni wabobezi wa taaluma mbalimbali na uzoefu wataweza kuisimimia mamlaka hiyo kufikia azma yake.

“Kila mmoja wetu hapa ana taaluma aliyobobea nayo, kwa mfano, tunao wataalam wa IT, wastaafu wa jeshi na wanasiasa…na muunganiko huo utaweza kuleta matunda mazuri kwa mamlaka,” amesema.

Wajumbe wa bodi mpya, imechukua nafasi ya bodi ya zamani ambayo muda wake ulimalizika Mei mwaka huu.

Wajumbe wa bodi ya sasa ni Simon Sayore, Brigadia Jenerali mstaafu Aloyce Mwanjile, Dk. Aikande Kwayu, Godfrey Leyla na Mhandisi Peter Ulanga.

Wengine ni Profesa Audax Mabula, Dk Fred Manongi, Profesa Kalunde Sibuga na mbunge wa zamani wa Namtumbo, Vita Kawawa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

error: Content is protected !!