Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Bocco aitwa Sauzi kumrithi Mbaraka
Michezo

Bocco aitwa Sauzi kumrithi Mbaraka

John Bocco
Spread the love

KOCHA Mkuu wa timu ya Taifa Tanzania, Salum Mayanga amemuongeza kwenye kikosi straika wa Simba, John Bocco kuchukua nafasi ya Mbaraka Yussuf aliyekuwa majeruhi, anaandika Catherine Kayombo.

Bocco ameshafika Afrika Kusini kujiunga na wenzake ambao wanatarajiwa kesho kushuka uwanjani kucheza mchezo wao wa Nusu Fainali ya michuano ya Baraza la Vyama vya Michezo Kusini mwa Afrika (Cosafa) dhidi ya Zambia.

Mshambuliaji huyo anachukua nafasi ya Mbaraka ambaye alipata majeruhi katika moja ya michezo yao ya awali ya kundi A, ambapo walikuwa pamoja na timu za Malawi, Mauritius na Angola.

Mayanga amesema amemuongeza Bocco katika kikosi hicho kwa malengo mawili, moja ni kujaza nafasi hiyo, lakini pia kuongeza nguvu kujiandaa na mchezo wao dhidi ya Rwanda wa kuwania kufuzu fainali za Kombe la Mataifa Afrika kwa wachezaji wanaochezea ligi za ndani (CHAN) zitakazofanyika mwakani nchini Kenya.

Mchezo huo unatarajiwa kufanyika Julai 15, mwaka huu kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza na marudiano yatafanyika mwishoni mwa mwezi au mwanzoni mwa Agosti.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

error: Content is protected !!