ROBERT Kyagulanyi maarufu Bobi Wine, amepinga matokeo yaliyotangazwa na Tume ya Uchaguzi ya Uganda mpaka sasa akidai hila zimefanyika. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).
Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 15 Januari 2021, Bobi Wine amesema, uchaguzi huo umetawaliwa na wizi wa kura huku akimtuhumu mpinzani wake ambaye ni rais wan chi hiyo, Yoweri Museveni kwamba, ameshiriki kuhujumu uchaguzi huo.
Kutokana na kudai kuwepo kwa wizi huo, ‘amejitangaza’ kuwa rais mteule wa Uganda. Mpaka sasa Museveni anaonga kwa zaidi ya asilimia 60 ya kura zote zilizohesabiwa.
Bobi Wine amesema, Taifa la Uganda limeshuhudia wizi mkubwa wa kura kuwahi kutokea, lakini hata hivyo hajaweka ushahidi wake wazi.
Pia amesema, hatua ya serikali kuzima intaneti imechangia kwa kaisi kikubwa kuvuruga matokeo ya uchaguzi huo huku akidai, mawakala wake wamekuwa wakikamatwa kwenye vituo vya kura.
Simon Byabakama, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi amemtaka Bobi Wine kuweka ushahidi wake hadharani juu ya madai yake ya wizi wa kura.
Amesema kuwa wagombea walikuwa na mawakala ambao walishuhudia kuhesabiwa kwa kura katika vituo vya kukusanya na kuhesabu kura.
Leave a comment