Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Bobi Wine amnyima usingizi Museven
Kimataifa

Bobi Wine amnyima usingizi Museven

Bobi Wine
Spread the love

Bobi Wine mwanamuziki wa miondoko ya pop na mwanasiasa wa upinzani nchini Uganda, anamnyima usingizi rais wan chi hiyo Yower Museven. Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Rais Museven yupo kwenye harakati ya kuhakikisha Bobi Wine ambaye jina lake halisi ni Robert Kyagulanyi Ssentamu hapati wasaa wa kukutana na waganda wenye uwanja wa siasa na muziki.

Dhamira ya serikali ya Museven imedhihiri jana baada ya kumkatalia kufanya tamasha lake leo lililopangwa kufanyika jana Disemba 26. Aliyetoa marufuku ya onesho hilo alikuwa Emilian Kayima, msemaji wa Jeshi la Polisi nchini humo.

Sababu iliyotolewa ni kwamba, Bobi Wine hakufuata utaratibu wa kisheria wa kuandika barua ya kuomba ruhusa ili aweze kufanya tamasha hilo.

Hata hivyo, gazeti la Daily Monitor la nchini Uganda liliandika kuwa, mapema leo jana Bobi Wine aliandika kwenye mtandao wa kijamii kuwa, kikosi cha usalama kimevamia tamasha lake la ‘One Love Beach in Busabala’na kuwakamata wafanyakazi wake.

Mwanzoni mwa mwezi Novemba mwanamziki huyo aliruhusiwa kufanya tamasha lake la kwanza kwa sababu lilikuwa la kiburudani na halikuwa la kisiasa.

Maelfu ya watu waliohudhuria tamasha hilo walivaa nguo nyekundu, rangi inayohusishwa na vuguvugu za Bobi Wine. Na pale alipopanga tamasha la pili, serikali imeamua kuzuia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!