Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Bilioni 985 zitakavyoboresha elimu ya juu Tanzania
Habari Mchanganyiko

Bilioni 985 zitakavyoboresha elimu ya juu Tanzania

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dk. Leonard Akwilapo
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania, kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia , imesema itatumia mkopo wa dola milioni 425 (zaidi ya Sh.985.49 bilioni), kufanya mageuzi na maboresho makubwa ya elimu ya juu ili kukuza uchumi kwa kuwa na wahitimu wanaoweza kuajirika na kujiajiri. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo Jumatano tarehe 13 Januari 2021 na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dk. Leonard Akwilapo jijini Dar es Salaam alipokuwa akifungua kikao kazi cha wadau cha kujadili rasimu ya miongozo  ya usalama wa mazingira na jamii katika utekelezaji wa mradi wa kuboreshaelimu ya juu  na mabadiliko ya kiuchumi (HEET).

Dk. Akwilapo amesema, fedha hizo ambazo ni Mkopo  kutoka Benki ya Dunia (WB) ulioidhinishwa katika mkutano wa tarehe 15 Desemba 2020, utajibu baadhi ya changamoto zilizopo katika vyuo vikuu

“Mradi unakuja kujibu baadhi ya changamoto, tunazokabiliana nazo katika vyuo vikuu nchini,” amesema Dk. Akwilapo.

Katibu Mkuu huyo amesema, miongoni mwa mambo yatakayotekelezwa katika mradi huo ni kuboresha na kujenga miondombinu mingine ya kufundishia na kujifunzia, kununua vifaa, kuhuisha mitalaa “ili kuwawezesha wahitimu kuajiliwa au kujiajili wao wenyewe.”

Amesema, mradi huo pia, utawezesha kuongeza udahili wa wanafunzi vyuoni kutoka ndani na nje ya nchi  huku akikumbushia kuwa zamani Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kilikuwa kikidahili wanafunzi wengi kutoka nje.”

Dk. Akwilapo amesema, kupitia mradi huo pia, wataalamu 639 watapata mafunzo na kutakuwa na mafunzo kazini ambapo vyuo 14 za umma vitahusika katika mradi huo.

Awali, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Profesa James Mdoe alisema, lengo la kukutanisha wadau ni kupata uelewa wa pamoja ili kushauri na kuboresha kuhusu mradi huo.

Profesa Mdoe alisema, mradi wowote unahitaji kuwa na rasilimali fedha na rasimali watu na ndiyo maana walianza kutafuta fedha kuanzia Januari 2018 na kufanikiwa kuidhinishiwa mkopo huo ambao ukianza kutekelezwa, utakuwa na matunda chanya kwa nchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

Habari Mchanganyiko

NMB yafuturisha Dar, Majaliwa azitaka Serikali za Mitaa, Taasisi zijifunze kwao

Spread the loveBENKI ya NMB imewafuturisha wateja wake walio kwenye Mfungo wa...

error: Content is protected !!