Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Biashara yampeleka Ally Kiba Coastal Union
Michezo

Biashara yampeleka Ally Kiba Coastal Union

Spread the love

NI wazi kuwa klabu ya Coastal Union imemsajili Msanii maarufu nchini Ally Kiba kwa sababu za kibiashara zaidi na uwezo wa staa huyo uwanjani. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Coastal imesajili Kiba katika kikosi chake kilichorejea Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kucheza ligi daraja la kwanza kwa misimu kadhaa iliyopita.

Mengi yameibuka baada ya Coastal kutangaza kikosi chake cha msimu huu, lakini swali la kujiuliza kocha wa kikosi hicho alimuihitaji staa huyo? Kiba atakuwa na muda wa kushiriki vizuri msimu mzima na kikosi hicho? Staa huyo yupo tayari kupumzika muziki na kujikita uwanjani? Uongozi wa Coastal utakuwa na majibu ya maswali hayo.

Ukichana maswali hayo, lakini inawezekana uongozi wa Coastal wameangalia kibiashara kwa kumtumia Staa huyo maarufu ‘Celebrity Marketing’ ambazo zinaweza kuinufaisha klabu kwa siku za mbele kutokana na ukubwa wa jina alilonalo mchezaji huyo ambaye pia ni mwanamuziki.

Uwepo wa Kiba unaweza kuwanufaisha Coastal kwenye upande wa mapato ya uwanjani, kutokana na mwanamuziki huyo kuwa na mashabiki wake binafsi, ambao wanampenda kutokana na kazi yake ya muziki hivyo watakuwa wanavutiwa zaidi kumuona uwanjani akicheza.

Lakini pia klabu yenyewe kama taasisi inaweza kuvutia wawekezaji wengi kuja kuwekeza kibiashara kutokana na kuwa na mchezaji mwenye ushawishi mkubwa ndani ya nchi na bara la Afrika kiujumla kutokana na yeye mwenyewe kuwa ni ‘Brand’ inayojitegemea.

Kama kungekuwa na utaratibu mzuri wa mapato wa haki za matangazo za televisheni basi Coastal Union ingenufaika kwenye hili kutokana na watu wengi watatamani kuifuatilia na kuitazama kwa njia ya televisheni timu hiyo kila inapo shuka dimbani kama zilivyokuwa Simba na Yanga.

Kwa upande wa mauzo ya jezi, Coastal wanaweza kutengeneza kiasi kikubwa cha fedha, kama kungekuwa na mifumo rasmi ya kibiashara ndani ya klabu za Ligi Kuu, sema kwa kuwa bado hatujajitambua na kujua tunataka nini kwenye soka, huu utajiri utaendelea kutupita tu.

Licha ya hayo yote lakini wadau wengi wa mchezo wa soka wanajiuliza ni namna gani Kiba ataweza kufanya kazi zote mbili kwa pamoja, kutokana na asilimia kubwa na umaruufu alioupata umetokana na kazi yake ya muziki ambayo ameifanya kwa zaidi ya miaka 10.

Na ukizingatia mchezo wa mpira unahitaji muda ‘Time Mnagement’ nguvu pamoja na mazoezi na muda huo huo aendelee kufanya shughuli zake za muziki ambazo naamini zinamuingizi kipato kikubwa kutokana na uhodari aliokuwa nao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!