Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Benki ya TPB, TIB Corparate zaunganishwa
Habari Mchanganyiko

Benki ya TPB, TIB Corparate zaunganishwa

Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imetangaza kuziunganisha Benki ya TPB na TIB Corparate kuanzia leo tarehe 1 Juni, 2020. Anaripoti Mwandishi, Dodoma … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo Jumatatu tarehe 1 Juni, 2020, Msajili wa Hazina nchini Tanzania, Athuman Mbutuka amesema, madeni na mali zote za TIB zitachukuliwa na TPB.

Amesema lengo la kuziunganisha taasisi hizo ni kuongeza ufanisi na kupunguza gharama, “ili kuwa na benki moja imara ya biashara. Muungano huu, utaleta mageuzi mkaubwa ya kiutendaji, muundo na taswira kwa ujumla ili iweze kushindana.”

“Kwa hatua hii tuliyofikia, Benki ya TPB inachukua mali na madeni yote ya iliyokuwa benki ya TIB Corparate na uamuzi huu, umeridhiwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT),” amesema Mbutuka

Amesema, Serikali itaendelea kusimamia utendaji wa benki zote ili  ziimarike kwa maslahi ya wateja.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!