TIMU ya Bayern Munich ya Ujerumani imetwaa ubingwa wa Ligi ya Mabigwa Bara la Ulaya (UEFA) kwa kuifunga PSG ya Ufaransa bao 1-0 lililofungwa na beki Kingsley Camon dakika ya 59. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea)
Katika mchezo huo, Bayern ilitawala karibu dakika zote 90 za mchezo huku wachezaji wa PSG Neymar, Mbappe na Di Maria wakishindwa kutumia nafasi walizopata.
Mlinda mlango wa Bayern, Manuel Never alifanya kazi kubwa kuokoa hatari zilizokuwa zikifanywa na washambuliaji wa PSG akiwemo Neymar, Mbappe na Di Maria.
Ubingwa huo wa Bayern ni wa sita na mara ya mwisho walitwaa taji hilo mwaka 2013.
Miaka mingine ambayo walitwaa ni 1974, 1975, 1976, 2001, 2013 na mwaka huu 2020.
Leave a comment