Tuesday , 19 March 2024
Home Kitengo Michezo Basila aahidi zawadi ya uhakika kwa mshindi
Michezo

Basila aahidi zawadi ya uhakika kwa mshindi

Basila Mwanukizi, Mkurugenzi wa kampuni ya Look LTD (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani)
Spread the love

BASILA Mwanukizi, Mkurugenzi wa kampuni ya Look LTD ambao ni waandaaji wapya wa Shindano la Miss Tanzania kwa mwaka 2018 amesema kuwa atahakikisha mshindi anapata zawadi ya gari inayostahili. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).

Mwanukuzi amesema hayo ikiwa hivi karibuni katika Shindano la Miss Lake Zone walikataa zawadi ya gari alilopewa nshindi huyo kwa kigezo cha kuwa halikustahili kupewa mrembo.

“Mrembo wa mwaka huu atapata gari zuri kabisa lakini ni vizuri ukampa gari zuri au usimpe gari kuliko kumpa gari ambayo ipo chini ya kiwango, ndiomaana gari ya kwenye mashindano ya Lake Zone tuliikataa kwasababu tuliona lazima tuwathamini warembo wetu, tumejiandaa vizuri na mrembo wetu atapata gari zuri tu na mtaliona,” amesema.

Hata hivyo Mwanukuzi amesema kuwa wao kama waandaaji wanahakikisha mambo kama ushindi kwa rushwa ya ngono, uvaaji ambao sio utamaduni wa kitanzania pamoja na mambo mbalimbali ambayo hayaleti picha nzuri katika tasnia hiyo ya urembo yanatoweka ili kurudisha hadhi ya shindano hilo.

“Sisi wote tubadilishe fikra tusirudi kwenye malalamiko na changamoto za nyuma tutakuwa hatusongi mbele, sisi ni kampuni mpya tupeane muda ili tuulizane changamoto zetu sisi kwakuwa hatuwezi kuzijibia changamoto zilizokuwa chini ya waandaaji wengine,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Tusua kijanja na mechi za Europa leo

Spread the love  Alhamisi ya leo EUROPA inaendelea ambapo ni mechi za...

Michezo

Hapa Diego Simeone, pale Simeone Inzaghi kivumbi cha Ligi ya Mabingwa Ulaya

Spread the love LIGI ya Mabingwa ulaya itaendelea usiku wa leo ambapoitakwenda...

error: Content is protected !!