DAKTARI Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar ametangaza Baraza la Mawaziri huku wizara mbili na nafasi ya manaibu waziri akiziweka kiporo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).
Akitangaza baraza lake leo tarehe 19 Novemba 2020, Rais Mwinyi amesema, katika wizara zake 15, wizara mbili ameziacha wazi akisubiri iwapo Chama cha ACT-Wazalendo kitaridhia kuunda Serikali ya Umoja wa Kimataifa (SUK) visiwani humo.
Yafuatayo ni majina ya mawaziri na wizara zao.
BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI ZANZIBAR:
1. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Uchumi na Uwekezaji – Mheshimiwa Mudrik Ramadhan Soraga.
2. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) – Mheshimiwa Masoud Ali Mohammed.
3. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Katiba na Utawala Bora – Mheshimiwa Haroun Ali Suleiman.
4. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango – Mheshimiwa Jamal Kassim Ali.
5. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Sera, Uratibu na Baraza la Wawakilishi – Mheshimiwa Dokta Khalid Mohammed Salum.
6. Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji na Mifugo – Mheshimiwa Soud Nahoda Hassan.
7. Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali – Mheshimiwa Simai Mohammed Said
8. Wizara ya Habari, Vijana na Utamaduni – Mheshimiwa Tabia Mwita Maulid.
9. Wizara ya Biashara ya Maendeleo ya Viwanda. Hakuna Waziri.
10. Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi – Mheshimiwa Riziki Pembe Juma.
11. Wizara ya Maji na Nishati – Mheshimiwa Suleiman Masoud Makame.
12. Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Watoto. Hakuna Waziri.
13. Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale – Mheshimiwa Lela Mohammed Mussa.
14. Wizara ya Uchumi wa Bluu na Uvuvi – Mheshimiwa Abdallah Hussein Kombo.
15. Wizara ya Ujenzi – Mheshimiwa Rahma Kassim Ali.
Leave a comment